Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Mwandishi wa habari wa jarida la Al-Wifaq amesema kuwa Shahidi Sayyid Ali Khamenei, kwa mtazamo wa wafuasi wake, hakuwa mtu ambaye simulizi yake imehitimishwa kwa kifo chake, bali ni kiongozi ambaye fikra, maadili na ujumbe wake vinaendelea kuishi na kuongoza vizazi vijavyo.

Katika makala yake yenye kichwa "Nyuma ya Kamera... Nilikuwa Nikitembea Tehran," Mwandishi huyo amesema kuwa Shahidi Sayyid Ali Khamenei ameingia katika hatua mpya ya athari na ushawishi wake, akisisitiza kwamba urithi wake unaendelea katika nyoyo za wafuasi wake.
Ameongeza kuwa, kama ambavyo kumbukumbu ya Imam Hussein (a.s) iliendelea kuwa hai katika dhamira ya Umma baada ya tukio la Karbala, ndivyo wafuasi wa Sayyid Ali Khamenei wanavyoona kuwa fikra na misingi aliyoiamini itaendelea kuishi na kuwa chanzo cha msukumo kwa vizazi vijavyo.

Your Comment